,

,

Wednesday, 27 November 2013

SHAHIRI; KITAMBI KIMENIPONZA


KITAMBI KIMENIPONZA

Kitambi kimeniponza,sina hamu asilani.
kimenifanya nawaza maisha si  ya thamani.
Mahari mara ya kwanza natakiwa milioni.
Wakashindwa kunioza kwa laki tano jamani.
Nikampenda shariza asili ya arabuni.
Ile tu kumposa dhahabu za milioni.
Ni kitambi sina pesa mi kabwela kama nini.
Kitambi kinaniponza nakosa mke jamani. 

No comments:

Post a Comment